12/30/12 | MIKENTOBI MIKENTOBI - A Blog with updated posts about events and current issues!
NEWS UPDATE :
Over a 100,000 ways to Earn Online!Sale Online!
[ New Posts ] : Habari Mpya Zote - HAPA CHINI!!!
Labels :

AIBU: TABIA YA KUPIGA PICHA ZA UTUPU YAENDELEA KUWATAFUNA AKINA DADA...!

Written By Mike Ntobi on Sunday, December 30, 2012 | 12:40 PM


AIBU.....AIBU.......

Tabia  ya  kupiga picha  chafu  za utupu  imeendela kuwatafuna  akina  dada  hapa  nchini.....

Tabia hii  ilianzia  kwa  wasanii maarufu kama  WEMA SEPETU,  JACK  WA  CHUZ,  LULU MICHAEL  RAYUU na sasa  imeingia  kwa  warembo wa  kawaida ......





Pamoja na jitihada za kuwaanika watu  hawa, tabia hii  imeendelea kuota mizizi kila kukicha.Wahusika wakuu wa  uchafu  huu ni akina dada.......

Iko haja kwa  akina  dada  kujitathmini.....Kwa  nini  kila siku ni wao tu???  Kwa nini  ukubali  kupigwa  ukiwa  mtupu  tena  na  mtu ambaye  mmekutana  na kupeana  penzi tu????....



Pengine ni  tamaa ya pesa.Nadhani hii ni biashara.Nashawishika  kuamini kuwa hawa  watu hupiga hizi picha kwa makubaliano maalum ya fungu flani la pesa.....



Nasema hivi maana  ni ngumu sana kwa mtu mwenye  akili zake  kukubali  kuaibika kisa  PENZI.

Na kama  ni tamaa  ya pesa, basi  haya  ndo matunda yake  maana  KILA  MTU HUVUNA  APANDALO.... 
--------------------------------------------------------------
NB:

Kuna  baadhi  ya  watu  wanalaum  kwamba hatujatenda  haki.Kabla  ya kulaumu jiulize yafuatayo:

1.Wasanii  wakikosea kila kitu huwekwa  hadharani  na hao  hao wanaolaum hushangilia.

2. Jiulize picha zimesambaa vipi?   wao ndo  waliozisambaza kwa sababu wakati  wa  starehe zao  walikuwa wawili tu chumbani.

3.Wema Sepetu akijiachia  wote  humponda kwa  kila aina  ya  tusi au neno baya.Tuache ushabiki.Haya  mambo hayafai

UOZO WA NORA WAANIKWA NA MUME WAKE.....!



MUME wa mcheza filamu mahiri za Kibongo Nuru Nassoro ‘Nora’, Masoud Ally ‘Luqman’ ameamua kuvunja ukimya baada mkewe huyo kueleza sababu zilizofanya ndoa yao kuvunjika ambazo anadai siyo za kweli. 

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Luqman ambaye alitumia zaidi ya saa mbili kutoa ufafanuzi kuhusiana na  habari hiyo, alikanusha vikali kuwa wazazi wake ndiyo chanzo cha kufanya ndoa yao ivunjike.

Alisema kuwa mama yake alikuwa akimpenda sana Nora mpaka staa huyo alikiri kuwa mkwewe huyo anampenda, sasa anaumia kumsikia akidai ndoa yake ilivunjwa na wazazi wake.



Luqman alizidi kutiririka kuwa katika maisha yake ya ndoa aliyoishi na Nora, amewahi kuwa na furaha mara mbili tu kutokana na ugomvi wa kila siku ambao mara nyingi ulikuwa ukisababishwa na Nora.

“Kiukweli ndoa yangu nakumbuka imewahi kuwa na furaha mara mbili tu lakini kipindi chote ilikuwa ni ugomvi usioisha,” alisema.


Aliendelea kusema kuwa kutokana na ugomvi wa kila siku,  kuna siku Nora alishika kiwembe na kumchana nacho mkononi, hali iliyosababisha ashonwe nyuzi tano.

Alisema kuwa alikuwa akijitahidi kujishusha ili kuinusuru ndoa yake kwa sababu bado alikuwa akimpenda sana mke wake huyo lakini hakufanikiwa na kwamba siku nyingine Nora alimshikia kisu kisa kikiwa ni meseji ambayo hakuituma yeye.


Aliendelea kuweka wazi kuwa kutokana na migogoro ya hapa na pale, alishampa talaka zaidi ya mara mbili na kumrudia tena akidhani labda atajirekebisha na kuwa sawa lakini haikuwa hivyo.



“Hii talaka ya mwisho niliyotoa ilikuwa ni ya tatu  lakini yote hayo ni kwa sababu nilimpenda sana mke wangu,”alisema na kuongeza kuwa waliamua kuhamia Zanzibar ambapo Nora mwenyewe alikupenda.

Hata hivyo, walipofika huko bado aliendelea kumsumbua na alijaribu kumtishia kuwa kama ataendelea hivyo ataoa mke mwingine ambapo kauli hiyo ilimkera Nora na kuamua kurudi Dar.


Alisema aliporudi Dar, mara kwa mara alikuwa akimsihi arudi wakaendelee kuishi lakini Nora alikuwa akikataa na ndipo alipoamua kuoa mwanamke mwingine ambaye kwa hivi sasa tayari wamezaa naye mtoto mmoja.


“Nilikuwa nikijaribu sana kumbembeleza Nora arudi ili tuendelee kuishi lakini hakuwa tayari ndipo nilipoamua kuoa mke mwingine,” alimalizia Luqman.

IRENE UWOYA ASHAREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUTOA MISAADA MBALIMBALI



Tofauti na mastaa wengine ambao huangusha party ya nguvu kusherehekea siku zao za kuzaliwa, hivi karibuni Irene Uwoya aliamua kufanya kitu tofauti katika siku yake ya kuzaliwa, December 18.

Muigizaji huyo mrembo aliamua kwenda kwenye hospitali ya Mwananyamala kutoa misaada mbalimbali kwa wagonjwa waliolazwa.

irene 4
irene 3
irene 2
irene 1

"NAJUTA KUTEMBEA NA MUME WA MTU"....TIKO



MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Tiko Hassan ‘Tiko’ amefunguka kuwa anajuta kutembea na mume wa mtu kwani majirani wanamuandama kwa maneno. 

Akizungumza na suala  hilo  juzikati jijini Dar, Tiko alisema kutokana na kuandamwa na maneno juu ya tabia hiyo ya kutembea na mume wa mtu  ameamua kutafuta mwanaume ambaye yupo singo.

“! Najuta mwenzangu. Bora nitafute mwanaume ambaye yupo singo waache kunisemasema kila siku,” alisema Tiko.

MZEE MAJUTO AJIPANGA KUTOKA NA "PATASHIKA" AMBAYO NI ZAIDI YA KOMEDI




MCHEKESHAJI mkongwe, Amri Athuman ‘King Majuto’ hivi karibuni ataanza kuonekana kwenye kazi mpya iitwayo “Patashika”


Katika kazi hiyo iliyojaa vichekesho vya kuvunja mbavu, Majuto atacheza kama baba wa familia mwenye vibweka vingi vya kustaajabisha, vinavyowaacha watu hoi kila siku mtaani kwao.

“Nategemea kufanya kitu cha tofauti ili mashabiki waweze kujua mimi ninaweza kuigiza ndiyo maana ninaigiza kama baba wa vibweka kwahiyo wadau wangu wategemee vimbwenga vya kustajabisha” alisema gwiji huyo wakuchekesha.

Mbali ya Majuto katika picha hiyo pia inawashirikisha nyota wengine ambao ni wakonnge kwenye Nyanja za uchekeshaji wakiwemo Pembe, Senga, Kingwendu, Full Tank na Difenda.

Kazi hiyo imepangwa kuingia sokoni hivi karibuni, ambako itapatikana mikoa yote hapa nchini, kwenye VCD pamoja na DVD.

"SIPO TAYARI KUZALISHWA KWA SASA"...BABY MADAHA



STAA wa filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha amefunguka kuwa hayupo tayari kuzaa kwa sasa.

Akizungumza kwa kujiamini, Baby Madaha aliweka wazi kuwa yupo bize sana na kazi zake za muziki na filamu hivyo suala la kunyonyesha litampotezea muda wake.

“We ubebe mimba sasa hivi, uilee halafu uje kunyonyesha, haya madili ya mjini yote yatafanywa na nani?” alihoji Baby Madaha na kuongeza:

“Mikakati yangu kwa mwaka 2013 ni kuhakikisha nafanya mapinduzi makubwa katika muziki wa Bongo Fleva na filamu.”

"NAWAPENDA MARAFIKI WA KIUME MAANA HAWANA MAJUNGU KAMA WANAWAKE".....QUEEN DARLEEN



STAA anayefanya poa na ngoma ‘Kokoro’, Queen Darleen, ameuambia mtandao huu  kuwa anajisikia raha kuwa na marafiki wengi wa kiume kuliko wanawake, huku akiamini kuwa tabia za baadhi ya wanawake ndizo zinazomfanya awe hivyo.

Msanii huyo ni mmoja ya wanawake wenye staili za kipekee kabisa kwenye game ingawa ndani ya mwaka huu amekuja kivingine kabisa baada ya kuwa kimya kwa muda na kuteka mashabiki kupitia kibao cha ‘Maneno Maneno’.

Kauli ya msanii huyo imekuja baada ya kuzungumza na mwandishi wetu alietaka kujua ni kundi gani la watu ambao hupenda kuwa nao karibu sana na kubandilishana mawazo ndipo yenye maana, ndipo alipofunguka kuwa mara nyingi huwa karibu na wanaume na si wanawake.

Alisema kuwa karibu na wanaume haimanishi kwamba ni mabwana zake hapana bali anaona ni watu ambao anaendana nao ingawa tabia zake si za kiume kama baadhi ya watu wanavyopenda kudhani kutoka na staili zake au aina ya kazi anazofanya.

“Kuna watu wanajua mimi nina tabia za kiume hiyo inawezekana kwa sababu wao ndo wanaosema, napenda sana kuwa na watu ambao tutafanya mambo ya maendeleo na si kuzungumza mapenzi na upuuzi muda wote hiyo ndo sababu kubwa inayonifanya nijiweke sana kwa wanaume,”alisema.

Hata hivyo aliongeza kuwa anahisi akijiweka karibu sana na wanawake hakuna kitu kikubwa watakachokuwa wanazungumza zaidi ya majungu na mapenzi, ingawa hata wanaume baadhi yao wako hivyo ila si kama wanawake ambao hupoteza mda mwingi kujadili ujinga.

“SCENES ZA MAPENZI KWENYE FILAMU ZINAWAUMBUA WASANII WANAONUKA MIDOMO” – IRENE UWOYA



MSANII wa filamu anayejichukulia umaarufu bongo Irene Uwoyaamedai kuwa kuna baadhi ya wasanii wenye majina makubwa wanapenda kucheza filamu za mapenzi na uchezeana huku wakishindwa kuelewa kuwa wananuka midono na mara nyingine huwa wanavumulia pasipo kutoa ukweli huo.

Kauli kama ya msanii huyu iliwahi kutolewa na Janet Jackson kwenye filamu ya ‘Poetic Justice’ iliyozinduliwa mwaka 1993 akimtaka Tupac Shakur kupima vizuri vya ukimwi kwani kuna kipande walitakiwa kuonekana wakipeana midomo kwani walicheza kama wapenzi ndani ya filamu hiyo, ndiyo kitu ambacho hata kwa wasanii wa kitanzania wanatakiwa kujifunza na si kukurupuka kupeana midomo..

Uwoya alisema kuwa kuna sehemu huwa wanakosea na kupeana midomo bila kupima afya kwani wapo wasanii wengine si wasafi na wananuka midomo huku wengine wakiwa wanatumia sana dawa za kulevya hivyo kuna hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa endapo wasipo chukua hatua.

Alisema kuwa wengine wanajijua walivyo lakini wanashindwa kujisafisha na kuwa katika hali nzuri badala yake ndani ya filamu wanaanza kupeanda kiss na kuchezeana bila kujua afya ziko vipi.

“Sasaivi naanza kuwa mkali kwa sababu endapo tukiendelea kuwa kimya tunaweza kujikuta magonjwa yanatukuta hivi hivi” aliongeza.

Hata hivyo msanii huyo aliwashauri baadhi ya wasanii wenye tabia za kupenda kupeana midomo ndani ya filamu wawe makini kwani huwezi jua ni ugonjwa gani anaoweza kupata, na kikubwa zaidi ni kupima kabla ya kazi kuanza ili kama kuna mtu mwenye tatizo apewe tiba mapema.

KUINGILIWA KINYUME NA MAUMBILE HAKUFAI......EPUKA KUJIZIBA MATAMBARA MAANA NI AIBU....!!!!!



Hii  ni picha  ya  mashoga ambao  bado  hawajitambui......Ni  jamii fulani  ya  watu  ambao UZUNGU  umewaponza.....

Ndugu  zangu,  ni  imani yetu  kuwa  jamii yetu  inahitaji kuelimishwa  sana ili tuweze  kuikomboa  mikononi mwa  hii  dhambi ambayo  ndo  dhambi kubwa  kuliko  zote......

 Tusipende  kuiga  kila kitu toka  kwa  WEUPE.Kabla  hujafanya maamuzi  yoyote Ni bora ukumbuke mambo yafuatayo:-
 
1. TIGO  Sio tendo asilia katika swala zima la ngono na mapenzi hivyo kumbuka unapoamua kugawa tako kuwa na uhakika ndio kitu unataka kukifanya na sio kukifanya kwa vile “mchumba” kaomba/anataka…..

Wewe ndio mwenye maamuzi makuu ya nini unataka kifanyike mwilini mwako. ........

  2.Mpaka  sasa  sidhani  kama  kuna kondom  imara yenye uwezo wakustahimili joto la huko "nyuma" .....

Kondom za kawaida  husababisha muwasho utakaoweza kukusababishia maambukizo mengine yatokanayo na wadudu asilia walioko sehemu hiyo ya haja  kubwa......

 3.Mara mishipa ya makalioni  ikitanuka kutokana na kufanywa huko mara kwa mara huwa haijirudi kama ilivyo kwenye uke kwa vile haikuumbwa kwa ajili ya shughuli hiyo.

EPUKA  KUJIZIBA  MATAMBARA....UTU  WAKO NI  BORA  KULIKO  HIYO  STAREHE  YA  DAKIKA CHACHE 

RIHANNA AJIACHIA TENA AKIWA MTUPU......



Picha za Mwanadada asiyeishiwa  vituko ( RIHANNA)  zimeendelea kusambaa kwa  kasi  katika  mitandao mbali mbali ya udaku.....

Picha hizo  zinazomuonesha  RIHANNA  akiwa mtupu  zilianza  kusambaa  kwa kasi jana mchana  na mpaka  sasa msanii  huyo  hajatoa kauli  yoyote kuhusiana  na picha  hizo.




KESI YA LULU MICHAEL YASAJILIWA RASMI MAHAKAMA KUU



Kesi ya mauaji ya kutokukusudia inayomkabili msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael `Lulu’, imepokelewa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kusajiliwa kwa namba 125 ya mwaka 2012.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana mahakamani hapo, kesi hiyo imepokelewa kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na inasubiri kupangiwa Jaji na tarehe ya kuanza kusikilizwa.

Awali Lulu alikuwa akikabiliwa na mashitaka ya kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba, kwa kukusudia lakini baada ya upande wa mashitaka kukamilisha upelelezi alibadilishiwa mashitaka na kuwa kuua bila kukusudia.

Kesi hiyo ilifunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu  Augustina Mmbando, katika hatua za awali na Lulu hakuruhusiwa kujibu mashitaka yanayomkabili kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Kwa mujibu wa sheria, kutokana na Lulu kushitakiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia, anaweza kupata dhamana.

"BABA YANGU ALIKUWA MVUTA BANGI NA AMEWAHI CHOMA MOTO NYUMBA YETU ILI AMUUE MAMA"....NICK MINAJ


Kila mtu ambae amefanikiwa kwa kupanda mwenyewe kutoka chini kwenda juu lazima anasimulizi la maisha yake ambalo lina mabonde na milima ya kushangaza kidogo, lakini inavuta usikivu na hisia sana pale msichana mrembo aliyefanikiwa kuwa kati ya list ya juu duniani kimuziki akiwa na simulizi la maisha yake linalotisha ama kuogofya tena akitishwa na yule aliyemzaa.



Jina lake la kuzaliwa ni Onika Tanya Maraj a.k.a Nicki Minaj, first lady wa Young Money mwenye umri wa miaka 30.



Nicki Minaj ali-experience maisha ya kusikitisha hasa katika familia yake mwenyewe iliyomlea, lakini pia mikiki mikiki toka kwa dingi mkorofi ilikuwa balaaa.
 Baba yake mzazi alikuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya kupitiliza, kiasi cha kuwa Teja ajabu, lakini pia alikuwa mkorofi na mkatili sana kitu kilichopelekea wanafamilia hao kuishi kwa uoga na mashaka.



Ilifikia hatua baba Nicki Minaj aliwasha moto kwenye nyumba ya familia hiyo akijaribu kumuua mama yake Nicki Minaj, jaribio ambalo halikufanikiwa.



Lakini Nicki Minaj mwenyewe anasema alijaribu sana kumsaidia mama yake kadri anavyoweza na alitaka awe shupavu sana lakini mama yake hakuweza, Nicki alijiwekea malengo ya kuwa mwenye mafanikio baada ya kufanya kazi ili amsaidie mama yake.



“Siku zote nilikuwa na hiki kitu cha kuwawezeshesha wanawake kwenye akili yangu”, aliliambia jarida la Details, “kwa sababu nilitaka mama yangu awe shupavu, na hakuweza. Niliwaza, kama ntakuwa mwenye mafanikio, Naweza kubadili maisha yake.” Huyo ni Nicki Minaj.



Nicki Minaj alianza kuandika mashairi akiwa na umri wa miaka 12 tu, na baada ya kumaliza La Guardia High School, ambayo inatoa elimu ya sanaa na Muziki aliwaza moja kwa moja kuingia kwenye biashara ya muziki. Alianzia chini na alianza kwa kufanya back up kwa rapperz wa jiji la New York.

Muda mfupi baadae alianza kuandika mashairi yake mwenyewe, na baadae akakutana na Lil Wayne aliyegundua kipaji chake ni silaha ya biashara ya muziki na kumsaini Young Money, ambapo alimsaidia kuifanya mixtape ya “Playtime is Over”, baada ya hapo akaishika dunia na michano yake na kuchukua tuzo kibao zenye heshima duniani, na kupata heshima pia hivi karibuni kuwa jaji wa shindano la kuimba la American Idol wakati album yake ya Pink Friday Roman Reloaded; Re-Up iko sokoni.

MABINTI WA VIDEO YA TYGA WAMSHITAKI KWA KUZIANIKA CHUCHU ZAO KINYUME NA MAKUBALIANO



Warembo watatu wanaonekana kwenye video ya ngoma ya Tyga’s“Make it Nasty” wanadai ‘chuchu’ zao zimeonekana bila ruhusa yao.


tyga-lawsuit



Alissa Rae Ross, Azia Davis, na Elizabeth Velasquez wamefungua mashtaka kwa kudai kuwa walipofanya usaili kwaajili ya video hiyo kulikuwa na kipengele kisemacho “There will be NO nudity involved in the video, and all the girls will be tastefully shot.”

Kwa mujibu wa madai yao Velasquez, Davis na Ross waliombwa wakati wa kushoot video hiyo July 2, kutokea wakiwa vifua wazi katika baadhi ya scenes lakini walihakikishiwa kuwa ‘chuchu’ zao zingefunikwa ama kufanyiwa editing.

Katika mkataba wao wasichana hao wanadai kuambiwa kuwa “drty” version ya video hiyo isingetoka lakini ikatoka. 
Wasichana hao wanashtaki kwa kukiuka mkataba, kuingiliwa usiri wao na madai mengine.

VITUKO VYA KRISMASI: NGUO ZA NDAN HADHARANI, SIGARA NA MADAWA YA KULEVYA KWA SANA


Mrembo  akiwa busy kuzikuna nyeti  zake bila kujali  watu....Kwake chupi  si kitu.Ionekane, au  isioneka  kwake ni sawa tu.....


Machangdoa nao hawakukosekana....Baadhi  yao walinaswa  wakipiga sigara na madawa  mengine ili kujipa  ganzi kwa  ajili  ya wateja  wao........

Kwa kifupi  ni kwamba, Mengi yametendeka wakati  wa sikukuu ya krismas.Kila mtu  aliamua  kutoka  kivyake  maadam  akidhi  haja zake......

 Neno  "machangu" ni la kawaida  siku hizi....Mwanamke  kuvuta  sigara  naona pia  wamelihalalisha.......

Jambo  la msingi ni kwamba TUKUMBUKE KUCHEZA SALAMA.....UKIMWI UPO NA UNAUA 
Get our toolbar!Get our toolbar!
  • Alexaporn - XXX (+18) Search!Alexaporn - XXX (+18) Search!
 
Sell Your Products At TripleClicks!Share Links Earn Money!
cafepress.com/nicemike
Sale Online!
Support : MIKENTOBI | Creating Website | Johny Template | Mas Template | UviOo | SFI

Copyright © 2010 - 2014. MIKENTOBI - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Modified and Published by MIKENTOBI
Proudly powered by Blogger