Laana!! Binti wa miaka 16 anaswa Akijiuza nyakati za Usiku Akiwa na mtoto mgongoni..!! | MIKENTOBI MIKENTOBI - A Blog with updated posts about events and current issues!
NEWS UPDATE :
Over a 100,000 ways to Earn Online!Sale Online!
Labels :
Home » , » Laana!! Binti wa miaka 16 anaswa Akijiuza nyakati za Usiku Akiwa na mtoto mgongoni..!!

Laana!! Binti wa miaka 16 anaswa Akijiuza nyakati za Usiku Akiwa na mtoto mgongoni..!!

Written By Mike Ntobi on Monday, January 27, 2014 | 11:16 AM

Binti (kulia) aliyenaswa akijiuza akiwa na mwanae jijini  Mwanza.

Ama kweli shida haina aibu wala huruma! Binti wa miaka 16 aliyetajwa kwa jina la Mama K, amenaswa laivu akifanya shughuli haramu za uchangudoa akiwa na mwanaye mgongoni, akidai chanzo cha kufanya hivyo ni kutokana na shida inayoiandama familia yake.

Binti huyo alibambwa hivi karibuni akijiuza huku mgongoni akiwa na mwanaye wa mwaka mmoja katika Barabara ya Uhuru (kwenye taa za kuongozea magari), jijini hapa.
Timu ya Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ambayo imetinga rasmi mkoani hapa ilinasa tukio hilo usiku wa manane ambapo ilifanikiwa kufanya mahojiano na Mama K aliyekuwa na wenzake wengi 
walio chini ya miaka 18.

Paparazi wa OFM akiwa kazini jijini Mwanza.


OFM ilichukua maelezo pamoja na picha za mnato huku wenzake wakitoka nduki baada ya kuona mwanga wa kamera.
Cha kushangaza, wakati akihojiwa na OFM, Mama K alidai kuwa haogopi  kupigwa picha kwa sababu alishanaswa na kuhojiwa runingani kuhusiana na ishu ya kujiuza hivyo siyo ishu kwake na wala haoni aibu.
Huku akiwa na mwanaye mgongoni, binti huyo alidai kuwa amekuwa akijiuza kutokana na ugumu wa maisha. 

OFM: Wewe unatokea maeneo gani na ulianza lini kujiuza? 
Mama K: Mimi ni mwenyeji wa Misungwi (wilaya), kwa hapa mjini naishi Mabatini. Sikumbuki nilianza lini lakini yote hii ni kutokana na ugumu wa maisha. 
OFM: Huyo mtoto mgongoni ni wa kwako? 
Mama K: Ndiyo ni mwanangu wa kumzaa, ana zaidi ya mwaka. Nilijifungua nikiwa na umri wa miaka 15. 
OFM: Baba wa mtoto yuko wapi? 
Mama K: Sijui. 
OFM: Ukipata mteja unamuweka wapi mtoto au unaenda kulala naye na mwanaume?
Mama K: (huku akiondoka) Nawaachia wenzangu.

Katika kujikusanyia data za kutosha, uchunguzi wa OFM uliogusa viunga mbalimbali jijini hapa ulibaini kuwa biashara hiyo haramu imeshika kasi ya ajabu ikihusisha vitoto vidogo kati ya umri wa miaka 12 hadi 16.
Kuhusu bei, tofauti na Dar ambako bei huwa ni ghali, jijini hapa vibinti hivyo vidogo hujiuza kwa kati ya shilingi elfu saba hadi kumi na tano kwa usiku mzima. Hakuna mambo ya 'short time'.
Katika kubainisha ukweli wa mambo kuhusiana na vitendo vya ukahaba ndani ya Jiji la Mwanza, OFM ilimtafuta meya wa jiji hilo ambapo simu yake ya mkononi haikupatikana hewani.

Akizungumzia na gazeti hili kuhusiana na ishu hiyo ya watoto wadogo kujihusisha na biashara hiyo haramu ya ngono, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo alikuwa na haya ya kusema:
"Sina taarifa yoyote kuhusiana na watoto hao wanaojiuza ndiyo nasikia kwako labda unipe muda niongee na uongozi wa chini nitalichukulia hatua mara moja.
Share this article :

Related Posts :

Post a Comment

 
Support : MIKENTOBI | Creating Website | Johny Template | Mas Template | UviOo | SFI

Copyright © 2010 - 2014. MIKENTOBI - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Modified and Published by MIKENTOBI
Proudly powered by Blogger