Serengeti Boys Kuivaa Misri | MIKENTOBI MIKENTOBI - A Blog with updated posts about events and current issues!
NEWS UPDATE :
Over a 100,000 ways to Earn Online!Sale Online!
Labels :
Home » » Serengeti Boys Kuivaa Misri

Serengeti Boys Kuivaa Misri

Written By Mike Ntobi on Wednesday, August 29, 2012 | 8:40 PM


RELEASE NO: 138
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

August 29, 2012

Timu ya Taifa ya Tanzania chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) sasa itaivaa Misri kwenye raundi ya pili ya michuano ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za 10 za Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

Awali Serengeti Boys ilikuwa icheze raundi ya kwanza dhidi ya Kenya, mechi ya kwanza ikichezwa Septemba 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) jana lilituma taarifa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) likielezea kujitoa kwenye michuano hiyo.

Serengeti Boys itaanzia nyumbani Oktoba 14 mwaka huu, wakati ya marudiano itachezwa nchini Misri kati ya Oktoba 26-28 mwaka huu. Mshindi baada ya mechi hizo mbili ataingia raundi ya tatu ambayo ndiyo ya mwisho kabla ya kwenda Morocco.

Katika raundi ya tatu ambayo mechi zake zitachezwa katikati ya Novemba na ya marudiano mwisho mwa mwezi huo, mshindi kati ya Tanzania/Misri atacheza na mshindi wa mechi ya Congo Brazzaville dhidi ya Msumbiji/Zimbabwe ambazo zinapambana katika raundi ya kwanza.

Wachezaji wanaounda kikosi cha Serengeti Boys chini ya Kocha Jakob Michelsen ni makipa Abdallah Bakar (Mjini Magharibi), Hamad Juma (Azam) na Peter Manyika (JKT Ruvu). 

Mabeki ni Abdallah Salum (Mjini Magharibi), Basil Seif (Morogoro), Hassan Mganga (Morogoro), Ismail Gambo (Azam), Mgaya Abdul (Azam), Miraji Selemani (Polisi Morogoro), Miza Abdallah (Kinondoni), Mohamed Hussein (Azam), Pascal Matagi (Dodoma) na Paul James (Kinondoni).

Viungo ni Farid Musa (Kilimanjaro), Hussein Twaha (Coastal Union), James Mganda (Kipingu Academy), Mbwana Ilyasa (Simba), Mohamed Haroub (Zanzibar), Mohamed Kapeta (Kinondoni), Mudathiri Yahya (Azam), Mzamiru Said (Morogoro) na Selemani Bofu (JKT Ruvu).

Washambuliaji ni Abdallah Kisimba (Mwanza), Calvin Manyika (Rukwa), Dickson Ambunda (Mwanza), Joseph Lubasha (Azam), Kelvin Friday (Azam) na Salvatory Nkulula (Kipindu Academy).

MCHEZAJI AOMBEWA ITC UJERUMANI
Chama cha Mpira wa Miguu cha Ujerumani (DFB) kimetuma maombi ya kupatiwa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Robert Makanja ili aweze kucheza mpira wa miguu nchini humo.

DFB imetuma maombi hayo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ili kumwezesha mchezaji huyo kuichezea timu ya TUS Ahausen, Hessischer FuBall-Verband ambayo hata hivyo haikuelezwa iko ligi ya daraja gani nchini humo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mashindano wa DFB, Markus Stenger, Mtanzania huyo ameombewa hati hiyo kama mchezaji wa ridhaa kwa maelezo kuwa hakuwahi kusajiliwa na klabu yoyote nchini.

TFF inafanyia kazi maombi hayo na hati hiyo itatolewa mara baada ya taratibu husika kukamilika ikiwemo kubaini kama kweli mchezaji huyo hakuwahi kusajili na klabu yoyote hapa nchini. 

Boniface Wambura Mgoyo
Afisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Share this article :

Related Posts :

+ Comments: + 7 Comments:

Anonymous
10:08 PM, September 12, 2012

These are truly enormous ideas in concerning blogging.
You have touched some good points here. Any way keep up wrinting.
Also see my site :: What is Penis Advantage

Anonymous
4:16 AM, September 19, 2012

always i used to read smaller articles that also clear their motive,
and that is also happening with this post which I am reading
now.
My web site blog link

Anonymous
3:09 AM, September 21, 2012

Since the admin of this site is working, no doubt very soon it will be well-known, due to
its quality contents.
Also visit my blog ; penis enlargement

Anonymous
4:05 PM, September 28, 2012

Good answer back in return of this question with real arguments
and telling everything regarding that.
Also visit my web site ... Hemorrhoid Miracle

Anonymous
5:36 PM, October 22, 2012

I quite like reading a post that will make men and women think.
Also, thanks for allowing for me to comment!
Look at my blog Alicia Pennington Scammer

Anonymous
1:07 PM, November 09, 2012

Just submit your email at http://www.freeipad3.allthebestproducts.
net and sign up to test Apple's products! You get to keep them afterwards!
My webpage > Click Here

Anonymous
12:25 AM, December 21, 2012

Good info. Lucky me I recently found your site by accident (stumbleupon).

I have book marked it for later!
Here is my homepage : Rick Nutile

Post a Comment

 
Support : MIKENTOBI | Creating Website | Johny Template | Mas Template | UviOo | SFI

Copyright © 2010 - 2014. MIKENTOBI - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Modified and Published by MIKENTOBI
Proudly powered by Blogger